KANISA KATOLIKI TANGA

this page in english

Mhashamu Askofu Maurus Komba, 1970 - 1988

 

Mhashamu Askofu Maurus Komba ni askofu mzalendo wa kwanza kuliongoza kanisa katoliki Tanga baada ya Askofu Eugene C. Arthurs, I.C.

Alizaliwa mwaka 1923 katika kijiji cha Mitambotambo katika wilaya Mbinga mkoa wa Ruvuma. Alipata elimu ya msingi katika shule msingi Litembo na baadaye alijiunga na shule za Peramiho na Kigonsera kwa masomo ya sekondari. Baadaye alijiunga na Seminari kuu ya Peramiho kwa masomo ya Falsafa na Teolojia. Alipewa daraja la upadre tarehe 15 Julai, 1954.
Akiwa padre alifanyakazi katika parokia za Mbinga, Mkumbi na Mbangamao katika jimbo la Mbinga na baadaye kama Paroko katika parokia ya Peramiho na Songea katika jimbo la Songea.

Aliteuliwa na Baba Mtakatifu Paul VI kuwa Askofu wa Jimbo la Tanga Machi 1969 na kuwekwa wakfu 15 Machi, 1970. Alifanyakazi kama Askofu wa Tanga kwa muda wa miaka 18 mpaka alipostaafu kwa sababu za kiafya mwaka 1987 na kurudi nyumbani kwao katika Jimbo la Mbinga. Alifariki 15 Machi 1996 na kuzikwa katika kanisa la parokia ya Mt. Alois Gonzaga, Mbinga.